Kadinali Protase Rugambwa aweka Historia Jimbo kuu la Tabora

Kadinali Rugambwa

Kardinali Protase Rugambwa Anaandika Historia ya Jimbo kuu la Tabora, Tanzania
Askofu mkuu Paul Runangaza Ruzoka wa Jimbo kuu la Tabora, Tanzania anaelezea furaha ya watu wa Mungu kwa kuteuliwa na hatimaye kusimikwa kwa Kardinali Protase Rugambwa, historia ya majimbo makuu ya Dar es Salaam na Jimbo kuu la Tabora na kwamba sasa Kardinali Protase Rugambwa anaandika historia mpya kwa maisha na utume wa Kanisa la Tanzania, kwa Jimbo kuu la Tabora kuwa ni Makao makuu ya Kardinali wa tatu nchini Tanzania. Tabora Kumenoga!
Na Padre Richard A. Mjigwa, C.PP.S. – Vatican.

Pichani kutoka Kulia, Kadinali Protuse, katikati Mheshimiwa Rais Dr. Samia Suluhu Hassani, na Kushoto ni Mhashamu Askofu Mkuu Paulo Ruzoka Tabora.

Baba Mtakatifu Francisko Dominika tarehe 9 Julai 2023 aliwateuwa Makardinali wapya 21 kati yao Makardinali watatu ni wale ambao wamejipambanua katika huduma kwa Kanisa na watu wa Mungu katika ujumla wao. Makardinali wapya wamesimikwa rasmi katika mkutano wa kawaida wa Makardinali tarehe 30 Septemba 2023 kwenye Uwanja wa Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican. Na tarehe 4 Oktoba Makardinali wapya wakashiriki katika Ibada ya Misa Takatifu kama sehemu ya ufunguzi rasmi wa Maadhimisho ya Sinodi ya XVI ya Maaskofu inayonogeshwa na kauli mbiu: “Kwa Ajili ya Kanisa la Kisinodi: Umoja, Ushiriki na Utume.” Makardinali kimsingi ndio walinzi wa imani na washauri wakuu wa Khalifa wa Mtakatifu Petro ili kukoleza juhudi za toba, haki, amani na maridhiano; kwa kukuza na kudumisha utu na heshima ya binadamu, ili watu waweze kuishi katika mazingira bora zaidi. Ukardinali umegawanyika katika ngazi kuu tatu: Kardinali Askofu, Kardinali Padre na Kardinali Shemasi. Katika mahojiano maalum na Radio Vatican, Askofu mkuu Paul Runangaza Ruzoka wa Jimbo kuu la Tabora, Tanzania anaelezea furaha ya watu wa Mungu kwa kuteuliwa na hatimaye kusimikwa kwa Kardinali Protase Rugambwa, historia ya majimbo makuu ya Dar es Salaam na Jimbo kuu la Tabora na kwamba sasa Kardinali Protase Rugambwa anaandika historia mpya kwa maisha na utume wa Kanisa la Tanzania, kwa Jimbo kuu la Tabora kuwa ni Makao makuu ya Kardinali wa tatu nchini Tanzania, sifa na utukufu apewe Mwenyezi Mungu.

Similar Posts

67 Comments

  1. After I initially commented I clicked the -Notify me when new feedback are added- checkbox and now every time a remark is added I get 4 emails with the same comment. Is there any method you may take away me from that service? Thanks!

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *