Mapokezi ya Mwadhama Polycarp Kardinal Pengo, Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu Katoliki Dsm, alipowasili Jimbo Katoliki Shinyanga katika ziara za kichungaji, mnamo tarehe 6.12.2023.
Katika picha ni baadhi ya waamini wa jimbo katoliki la Shinyanga wakiwa na nyuso za furaha wakimkaribisha Kardinali Pengo katika mipaka ya jimbo hilo
Mha Askofu Sangu aongoza mapokezi na kumkaribisha Mwadhama kadinali Pengo jimboni humo kwa ziara ya kichungaji kuanzia tar 06.12.2023
Dominika ya Sita Ya Mwaka B wa Kanisa: Siku ya 32 ya Wagonjwa Ulimwenguni 2024 Maadhimisho ya Siku ya 32 ya Wagonjwa Ulimwenguni yananogeshwa na kauli mbiu “Si vizuri kwamba mwanadamu awe peke yake. Uponyaji wa wagonjwa katika kuponya mahusiano.” Baba Mtakatifu anaangalia vita kama gonjwa kubwa na la kutisha, uzee na upweke. Kumbe, kuna…
Usaili kwa kidato cha kwanza ni tarehe 3_4 January 2024 kutakuwa na mitihani. Kwa wanaohamia mitihani ya usaili ni December 2023 wazazi wa wahi nafasi ni chache, Asante kwa USHIRIKIANO wako, Mungu azidi kukubariki daima.
Baba Mtakatifu Francisko Ijumaa tarehe 5 Aprili 2024 amekutana na kuzungumza na Jumuiya ya Ndugu Wadogo wa La Verna na wale wanaotoka Kanda ya Toscana, kama sehemu ya kumbukizi ya miaka mia nane tangu Mtakatifu Francisko wa Assisi alipobahatika kupewa Madonda Mtakatifu mwilini mwake. Hii ilikuwa ni tarehe 15 Septemba 1224, yaani miaka miwili kabla…
Mama Kanisa katika masomo ya dominika hii anatukumbusha kuwa kwa Sakramenti ya Ubatizo na kipaimara sisi sote tumeitwa kuihuburi Injili kwa kuishi ukristo wetu vyema sio kwa sheria za maumbile bali kwa kuwa viumbe vipya ndani ya Kristo na kuona fahari juu ya Msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo ambao kwao tumekombolewa. Hii ni changamoto…
Na Padre Joseph Herman Luwela, – Vatican. Nyumba ya Baba yangu ni nyumba ya sala, toba na wongofu wa ndani na sio genge la biashara huria! Leo Kanisa linaadhimisha Dominika ya 3 ya Kipindi cha Kwaresima Mwaka B wa Kanisa. Himizo kubwa katika kipindi hiki cha Kwaresima ni toba na wongofu wa moyo na muunganiko…
Kipindi cha Kwaresima ni fursa ya kuamsha na kupyaisha ari na mwamko wa kimisionari, tayari kujisadaka bila ya kujibakiza kwa ajili ya kutangaza na kushuhudia Habari Njema ya Wokovu hadi miisho ya dunia. Baba Mtakatifu Francisko anawaalika waamini kuwakumbuka na kuwaombea wainjilishaji wote, ili waweze kuwa ni vyombo na mashuhuda wa kile wanacho amini, kufundisha…