Tarehe 07.12.2023 mwaka wa Bwana katika nyumba ya malezi parokia ya Chala
Katika picha ni Masista 16 wa nadhiri za kwanza wa shirika la Maria Mtakatifu Malkia wa Afrika-Jimbo la Sumbawanga 07.12,2023
Adhimisho la Misa Takatifu limefanyika katika Kanisa la Nyumba ya malezi ya Shirika hilo, iliyopo Parokia ya Mtakatifu Fransisco wa Sales – Chala Jimbo Katoliki Sumbawanga. Ikiwa ni utangulizi wa sherehe za Shirika hilo, ambazo hufanyika tarehe 08.12. au maarufu Nane Disemba Sherehe ya Bikira Maria Mkingiwa dhambi(Emakulata).
Adhimisho la Misa Takatifu limeongozwa na Askofu Emeritus Damian Kyaruzi wa Jimbo la Sumbawanga, Na aliyepokea Nadhiri 16 za kwanza kwa Masista 16 ni Mama Mkuu wa Shirika hilo Mheshimiwa SR. Editruda Mbegu Mbele ya Mhashamu Baba Askofu Damian Kyaruzi, ambaye amemwakilisha askofu wa Jimbo Mha, Beatus Urassa ALCP/OSS.
Katika sherehe hizo za nadhiri za kwwanza wameudhuria , watu mbalimbali wakiwemo mapadri, watawa waamini wakinogeshwa na furaha ya walelewa amabo wameshuhudia safari ya dada zao ikifika mwisho katika hatua msingi ya nadhiri za awali tunawaombea udumifu mwema
Katika picha hapo chini ni mnadhiri mpya wa nadhiri za kwanza Sista Maria Nzunda kutoka parokia ya Tunduma jimbo katoliki Sumbawanga
Na. Pd Joseph Luwela-Vatican-Roma Utakatifu ni mchakato unaowawezesha waamini kuishi upendo katika utimilifu wake kadiri ya nguvu na mwanga wa Roho Mtakatifu. Maisha ya kila mwamini yawe ni kielelezo cha utume kutoka kwa Kristo Yesu anayetaka kuwaletea waja wake mabadiliko katika maisha, licha ya udhaifu na mapungufu yao ya kibinadamu, daima wakijitahidi kuambata upendo wa…
Na Padre Joseph Herman Luwela, – Vatican. Nyumba ya Baba yangu ni nyumba ya sala, toba na wongofu wa ndani na sio genge la biashara huria! Leo Kanisa linaadhimisha Dominika ya 3 ya Kipindi cha Kwaresima Mwaka B wa Kanisa. Himizo kubwa katika kipindi hiki cha Kwaresima ni toba na wongofu wa moyo na muunganiko…
Mapokezi ya Mwadhama Polycarp Kardinal Pengo, Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu Katoliki Dsm, alipowasili Jimbo Katoliki Shinyanga katika ziara za kichungaji, mnamo tarehe 6.12.2023. Katika picha ni baadhi ya waamini wa jimbo katoliki la Shinyanga wakiwa na nyuso za furaha wakimkaribisha Kardinali Pengo katika mipaka ya jimbo hilo
Baba Mtakatifu Francisko anasema, huruma ndiyo msingi thabiti wa uhai wa Kanisa. Kazi zake zote za kichungaji zinapaswa kufungamanishwa katika upole linalouonesha kwa waamini; hakuna chochote katika mahubiri na ushuhuda wake kwa ulimwengu kinachoweza kukosa huruma. Umahiri wa Kanisa unaonekana kwa namna linavyoonesha huruma na upendo. Huruma ya Mungu inafungua malango ya moyo ili kuonesha…
Usaili kwa kidato cha kwanza ni tarehe 3_4 January 2024 kutakuwa na mitihani. Kwa wanaohamia mitihani ya usaili ni December 2023 wazazi wa wahi nafasi ni chache, Asante kwa USHIRIKIANO wako, Mungu azidi kukubariki daima.
Mama Kanisa katika masomo ya dominika hii anatukumbusha kuwa kwa Sakramenti ya Ubatizo na kipaimara sisi sote tumeitwa kuihuburi Injili kwa kuishi ukristo wetu vyema sio kwa sheria za maumbile bali kwa kuwa viumbe vipya ndani ya Kristo na kuona fahari juu ya Msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo ambao kwao tumekombolewa. Hii ni changamoto…